BOSI ANANITAKA NIWE MCHEPUKO WAKE ---- 01
BOSI ANANITAKA NIWE MCHEPUKO
WAKE
SIMULIZI BUNILIZI
MTUNZI: Mwl Juma
WhatsApp: 0762957992
Sehemu ya 01.
Ilikuwa siku ya alhamisi asubuhi nilipogutuka kutoka usingizini baada ya
ndoto niliyokuwa nikiiota kukatika ghafula bila kutambua nilichokuwa nikikiota.
Nilishirikisha halmashauri ya kichwa changu kilichochongoka kwa mbele mithili
ya treni ya umeme yenye kutumia gesi asilia bila kupata jawabu lolote na kubaki
nimeduwaa kama mfalme wa Babeli akitegemea tafsiri ya ndoto yake pasina
kuambulia chochote. Niligundua ilikuwa imefika saa mbili asubuhi baada ya kuona
mwanga wa jua uliopenya kwenye ufa mpana wa kona ya kijumba nilichokuwa nimelala
kwa muda.
Niliamka na kupiga mswaki halafu nikavaa t-shirt rangi ya bluu, suruali ya
kadeti rangi ya kaki na raba rangi nyekundu miguuni kisha nikajichanganya
mtaani nikihangaika huku na kule mithili ya kuku aliyekatwa kichwa akicheza
dansi la kukata roho huku akiisaliti suruali yake na kutaka avae kaptura ikiwa
ni harakati za kuzisaka noti zilipo bila kusahau bahasha yangu mkononi iliyokuwa
imebebea vyeti na baadhi ya matini ngumu(hardcopies) zinazonihusu. Nilibisha
hodi kila ofisi niliyodhani pengine ningebahatisha kupata kazi kulingana na
taaluma yangu niliyoisomea ya komputa kwa ngazi ya shahada katika chuo fulani
maarufu hapa nchini. Juhudi zangu ziligonga mwamba siku kwa siku bila kupata
kazi nikahisi kukata tamaa ya maisha kwani hata pa kuishi nilikuwa nikikaa kwa
rafiki yangu ambaye pia noti zimemsaliti.
Niliendelea kuishi na rafiki yangu aitwaye Edward huku nikipendelea kukaa
kibarazani nikiwa na simu yangu ya Tecno W3 nikizikagua arafa zilizozituma kwa
marafiki zangu niliosoma nao chuoni pasipo mrejesho wowote ikiashiria hawana
hata pesa ya kununulia msosi wa buku sembuse kuunga bando la SMS ni ndoto.
Nilizidi kukata tamaa na kujisemea moyoni kuwa kama ni mbwai wacha iwe mbwai
nitajiingiza hata kuuza kete za mirungi na wahuni wa mtaa angalau nisavaivu
bila kujali ni biashara haramu.
Siku iliyofuata mida ya jioni nilijiandaa kwa mitoko nikazurure mtaani,
nilivaa dizaini ya kimagharibi yaani pensi rangi nyeusi yenye mistari miyekundu
mapajani, t-shirt fulani ya kijanja pamoja na earphone masikioni kisha
nikajichanganya mtaani kushangaa shangaa mji kama njia ya kupunguza mawazo.
Ghafula nilipokuwa njiani nilisikia honi ya gari iliashiria nipishe gari
ipite nilipogeuka ilikuwa ni gari ndogo nyeusi aina ya LANDCRUISER. Nilipisha njia lakini cha kushangaza gari lile liliponipita
tu lilisimama wakati huo mapigo yangu ya moyo yapiga kwa kasi mithili ya moyo
kuruka kichurachura nikajawa na wasiwasi mkubwa na kujiuliza sababu ya gari lile
kusimama mbele yangu na kukosa pa kupitia kwani njia ilikuwa ya kawaida isiyo
rasmi.
Dereva alishusha kioo cha dirisha kumbe alikuwa ni mwanamke aliyekuwa
akiendesha gari. Mwanamke huyo alinisalimia akisema “mambooo...” nikamjibu “poa tu
mama shikamoo” aliitikia salamu yangu kwa shingo upande kama vile
kuipotezea akajibu tu “usijali mimi niko
poa” lakini vipi unaelekea wapi?
Aliniuliza mwanamke yule nikamwambia “naelekea
mtaa wa pili”. Mwanamke yule nisiyemfahamu vizuri aliniomba sana niingie
ndani ya gari lake anisogeze mtaa ninaoelekea. Ilibidi nikubali, nikaingia
ndani ya gari kisha mdogo mdogo gari likaondoka.
Nilijiuliza maswali mengi kichwani mwangu yasiyo na majawabu kuhusu huyu
mwanamke maana simfahamu lakini ananichangamkia kama vila tunajuana. Ukimya
ulitawala kati yetu takribani dakika mbili huku nikimtazama kiwiziwizi kwa
kumzoom hakika mwanamke yule alikuwa mzuri sana mwenye umbo la aina yake
sijawahi kukutana na mwanamke mzuri kama huyo ingawa nilihisi aibu na
kuchanganyikiwa kwa jinsi alivyovaa kimitego kumnasa kuku wa kienyeji aliye
karibu naye.
Mwanamke yule nisiyemfahamu kwa kumwangalia tu alikuwa na umri unaokadiriwa
kati ya miaka 28-35, ana umbo zuri la namba nane, mshale wa matiti yale unasoma
saa sita na robo kabla ya muda wa kuhangaika kutegesha redio kusikiliza kipindi
cha dira ya dunia ya saa saba kutoka Ujerumani, ana miguu mizuri hakuna mfano
wake, sauti yake inamfanya nyoka aingie pangoni mwenyewe badala ya kutoka,
kiuno chake kinamvutia jogoo kuwika muda wowote bila kujali ni muda gani, lips
zake hazina mfano ameumbwa akaumbika. Baada ya ukimya mfupi aliamua kunisemesha
“vipi unaonekana wewe ni kijana mtaratibu
sana huwa nakuona kila siku umekaa kibarazani nikipita na gari yangu kuelekea
kazini” nilishtuka sana kumbe yule mwanamke huwa ananiona kila siku lakini
mimi simfahamu. Aliniomba anipeleke nyumbani kwake nipafahamu kwani ni mtaa wa
pili jirani na ninakoelekea kupiga misele yangu.
Mwanamke yule alijitambulisha kwangu akasema anaitwa Rebecca ni mmiliki wa
kampuni ya kuuza vipodozi ambavyo huziuzwa hadi nje ya nchi lakini ana ofisi
yake kama bosi wa kampuni yenye wafanyakazi kedekede. Nilijiuliza maswali
kichwani mwangu bila majawabu kuwa ni kwanini sasa bosi mkubwa kama huyu
ananitegatega na vinguo vyake anakaa nusu uchi akijifunua funua makusudi ili
nimwone pia niligundua kuwa Rebecca ana uwezo mkubwa kiuchumi sasa inakuwaje
anahitaji kujuana na kapuku kama mimi? ambaye sina hata mia mfukoni bali
umaskini wangu unafichwa tu na pamba ninazopiga utadhani nina mkwanja. Nilijikaza
kiume nikajisemea moyoni endapo ananitaka sitapoteza fursa hii adimu kwa
mwanamke aliyeumbika kama huyu lazima nimwandikie dozi iliyochanganywa na
glukosi itakayotibu ugonjwa wake kisawa sawa akijilengesha kwangu. Tulifika
nyumbani kwa Rebecca akapiga honi geti likafunguliwa akaingiza gari.
Alinikaribisha niingie naye ndani ya nyumba yake kitu ambacho hata mlinzi
wake hajawahi kufanyiwa kuinusa hata sebule. Mlinzi alishangaa sana kuniona
nakaribishwa ndani kwa bosi Rebecca.
Rebecca ana nyumba nzuri ya kifahari yenye fulu kiyoyozi pazuri hakuna mfano
wala sijawahi kuingia kwenye nyumba kama ile. Rebecca alikaa kwenye kochi mojawapo
huku mimi nilibaki nikizidi kushangaa nyumba ilivyo nzuri nikiwa nimesimama
kwanza kwa woga huwezi kuamini lakini nikapiga moyo konde nikajisemea moyoni
kuwa sitakiwi kuogopa mimi kama kidume.
Rebecca alinitazama akaniambia “jamani
handsome mbona umesimama naomba ukae usiogope mimi ndo mwenye nyumba hakuna
mwingine” ndipo nikakaa kwenye kochi lingine lakini Rebecca alitaka nikae
karibu yake kitu ambacho nilikuwa nakihofia nikijiuliza kichwani nini kusudi la
huyu mwanamke ingawa ilibidi niondoe woga kwa sababu nimeshatambua
anachokihitaji kutokana na mitego yake kujifunua funua kiasi kwamba msambwanda
wake upo nje nje duuuh nilikaza roho.
Niliamka nilipokuwa nimeketi nikakaa karibu yake kama anavyotaka nikae
karibu yake, akaniwekea mkono wake wa kulia kwenye bega langu nilisisimka mwili
mzima ghafula tukatazamana naye kwa sekunde kama ishirini hivi. Akaanza kuongea
kimahaba huku macho yake yamelegea akiniambia leo nitakupatia zawadi naomba
uipokee wewe ni handsome wangu nitakupa kila unachokihitaji kutoka kwangu
tulianza kuzawadiana mabusu moto moto nilijihisi matatizo yangu yamesahaulika
kwa muda huo.
Alinichangamkia kama Mangi amemwona mteja ikabidi nioneshe ushirikiano
nikiyapapasa makalio yake makubwa yaliyojaa jaa na kuonekana mithili ya kichuguu
kilichojengwa na mchwa mafundi waliosomea ufundi washi. Nilianza kuyanyonya
matiti yake yaliyoumbwa yakaumbika tukiwa palepale kwenye kochi ndipo Rebecca
alipoanza kuhema kwa kasi. Niliupeleka mkono wangu taratiiibu kuanza harakati
za kuisaka ikulu yake ndogo iliyozungushiwa fensi imara nilipoigusa nilimsikia akilalamika
kwa sauti ishiiiiiiiiiiii uwiiiiiiii jamani handsome wangu utaniua kwa raha hizi naomba uhamie kwangu aliropoka.
ITAENDELEA................................................
Fuatilia sehemu ya pili kujua
kilichoendelea...........................................................................
Guuud work @Mwljuma
ReplyDeleteEnter your comment...simulizi nzuri sanaa
ReplyDeleteEnter your comment...hii story tamu sanaa nitaipataje yote @mwl juma na gharama zake vipi
ReplyDeleteAhsante Carine njoo inbox
DeleteAhsante Carine njoo inbox
Delete